NAFASI ZA MASOMO KWA KIDATO CHA KWANZA MWAKA: 2026 NA KIDATO CHA TANO (FV) MWAKA 2025/2026;
Uongozi wa Shule ya Sekondari Maria De Mattias inayopatikana Kisasa “B” Manispaa ya Dodoma, unawatangazia wazazi/walezi wote nafasi za masomo kwa Kidato cha kwanza kwa mwaka 2026 na kidato cha tano kwa mwaka wa masomo 2025/2026.
- Kidato cha Tano (FV) nafasi bado zipo kwa Tahasusi (Combination) zifuatazo:
- PCB, PCM, CBG, PGM, EGM, HGE, HGL na HKL.
FOMU ZA KUJIUNGA
Fomu za kujiunga kidato cha kwanza mwaka 2026 na kidato cha tano (FV) kwa mwaka wa masomo 2025/2026 zinapatikana maeneo yafuatayo kwa gharama ya Tsh. 20,000/= tu.
- Shuleni Maria De Mattias (Dodoma).
- Katika tovuti yetu ya shule ambayo ni: www.mariademattiassec.sc.tz.
- Morogoro, kwa Masista Waabuduo Damu ya Kristo (Kola B): 0762987474.
- Dar es Salaam, Mbezi Beach-Tangi Bovu kwa Masista: 0628291000.
- Dar es Salaam, Msimbazi Center Chumba namba 22. 0715265446.
- Moshi Bookshop (Kilimanjaro).
NAMNA YA KUJIUNGA
Usaili (interview) utafanyika tar 16/09/2025 shuleni Maria De Mattias (Dodoma) na Mbezi Beach Tangi Bovu (Dar es Salaam).
Muda wa kuripoti kituo cha mtihani ni saa moja kamili asubuhi.
NB: Shule ya Sekondari Maria De Mattias ni shule ya Bweni kwa O-LEVEL na A-LEVEL na ni ya wasichana tu.
“Mlete mwanao Maria De Mattias Sekondari kwa Elimu na Malezi bora”.